Tunapatikana Sinza kwa Remmy

Tunapatikana Sinza kwa Remmy

Thursday, June 5, 2014

ADHABU KWA MKE KWA KUMTELEKEZA MUME



Mwanamke mmoja nchini Kenya ameamrishwa na mahakama kumlipa mumewe shilingi elfu tatu au dola 35 kama hela za kukidhi mahitaji yake na watoto wake kila mwezi.
Mwanamke huyo kwa jina Roselyn Muyonga, ambaye anatuhumiwa kwa kuwatelekeza mumewe na watoto wake watatu , huenda akafungwa miezi mitano jela au kutozwa faini ya shilingi laki mbili ikiwa atakosa kutekeleza amri ya mahakama.

Mwanamume huyo hufanya kazi za kibarua.
Afisaa mmoja wa watoto katika jimbo la Kakamega Magharibi mwa Kenya, alisema kuwa mwanamke huyo alipuuza jukumu lake la kulea watoto wake baada ya yeye na mumewe kutalakiana.
Afisa huyo alisema kuwa wanaume huachiwa majukumu mengi sana wakati wanapoachwa na watoto na kwamba wanawake kama Roselyn wanapaswa kuamrishwa kuwatunza watoto wao hata kama wameachana na waume zao.
Tayari mashirika kadhaa yanataka kushinikiza sheria ya kuwashurutisha wanawake kutoa mchango kwa kuwalea watoto wao wanapoachana na mwanamume au baba ya watoto.
Kwa mujibu wa afisaa mmoja wa watoto, visa vya wanawake kuwatelekeza watoto wao katika jimbo hilo vimeongezeka.
chanzo BBC 

HAYA KAZI KWENU WAPENDA KUONYESHA MIILI YENU HADHARANI INSTAGRAM YAFUTA PICHA ZA UCHI



Mmoja wa waasisi wa mtandao wa kijamii wa Instagram, ameambia BBC kuwa sheria zake kuhusu picha za uchi hazimbagui mtu yeyote.
Kampuni hiyo imekosolewa vikali kwa kwa kuondoa picha za wanawake walio nusu uchi kwenye mtandao huo.

Lakini Afisaa mkuu mtendaji wa mtandao huo wa kijamii, Kevin Systrom, amesema kuwa sheria hizo zinalenga kuhakikisha kuwa vijana na watu wazima wanaotumia mtandao huo wako salama.
Masharti ya matumizi ya mtandao wenyewe, yanasema: 'Mtu haruhusiwi kuweka picha za watu walio nusu uchi na picha zenye mada ya ngono. ''
Matamshi yake yanakuja baada ya mwanawe muigizaji maarufu, Bruce Willis, Scout Willis kuweka picha yake kwenye mtandao huo akiwa nusu uchi bila kitu kifuani.
Picha hiyo iliondolewa kwenye mtandao huo na wamiliki wa mtandao na hapo ndipo malalamiko yalianza kuibuka.

Muimbaji Rihanna, ambaye alikuwa na wafuasi milioni 1.3 aliunga mkono kampeini hiyo kabla ya kufunga akaunti yake.

Wamiliki wa mtandao huo wanasema sheria zinapaswa kufuatwa na kila mtu awe mtu mashuhuri au vinginevyo.

"lengo letu ni kuhakikisha kuwa Instagram, ni mahala salama kwa kila mtu , awe maarufu au la. ''
"tunapaswa kuwa na sheria na kuhakikisha kuwa kila mtu anafuata sheria hizo. Bila shaka tunapata changamoto nyingi lakini tutnaedneklea kusisitiza umuhimu wa sheria kufuatwa, '' alisema Systrom
Huku umaarufu wa mtandao huo ukiendelea kuimarika, mtandao huo umekosolewa kuhusiana na baadhi ya picha zinazochapishwa humo . Pia mtandao wenye umebana baadhi ya maneno yanayohusiana na madawa ya kulevya.
Instagram ilinunuliwa na Facebook mwaka 2012.

Chanzo cha habari BBC swahili.

Wednesday, June 4, 2014

NATHALIE MAKOMA NI NANI MFAHAMU WALAU KWA UFUPI TU !




 Hebu kwanza kabla hatujaenda kumtazama na kumfahamu angalia wimbo huu alioweza kuimba na mwanamuziki mkongwe wa muziki wa dansi bonge moja ya rumba Nathalie Makoma akiwa na Papa Wemba wanakuambia Six millions ya ba soucis ...kisha nitakujuza zaidi.

<iframe width="640" height="390" src="//www.youtube.com/embed/ljEtJYGRxGg" frameborder="0" allowfullscreen></iframe>

Naaam Nathalie makoma sio jina geni sana kwenye ulimwengu wa muziki wa gospel kwasababu ndiko alipotokea mwana dada mahiri mwenye sauti ya kipekee kutoka jamhuri ya kidemokrasia ya kongo.. alijulikana mmo wakati alipoachia kibao cha Nzambe na Bomoyi (Jesus For Life) wakati huo wakiwa waimbaji kwaya wanafamili anzima ya Makoma.
Nathalie Makoma, alizaliwa huko  Kinshasa, Zaire February 24, ya mwaka 1982, ni mwambiji wa ambae amekulia kwa wa  Dutch slakini mwenye asili ya kongo. 


Wazazi wake  wote wanatoka  ni wenyeji wa jamhuri ya watu wa  Congo. She alikuwa muimbaji kiongozi katika kundi la Makoma kabla ya kujiengua na kuwa mwanamuziki wa kujitegemea yani solo artiest 
mwanadada huyu amewahi pia kushiriki katika mashindano mbalimbali ya uimbaji ikiwemo lile la Dutch Idols shindano ambalo lilimpeleka mpaka hatua ya  nne bora singing competition in its fourth season reaching the final and finishing as runner-up toshindano ambalo naweza kusema kwamba lilimfungulia milango na hatimae kuingia mkataba na makampuni makubwa sana yaliomfanya aanze kutengeza fedha ikiwemo lile la  Sony BMG. .

Nathalie Makoma  alianza kuimba  akiwa na kundi la familia yao 1993 alipokuwa na umri wa miaka 7 tu   wakati ambapo bendi yao ilijulikana kwa jina la "Nouveau Testament". kisha baadae kubadilishwa jina na kuitwa  Makoma  kundi ambalo liliundwa na wanafamilia wapatao saba (7)  wakiwa kaka zake watatu na kijana mmoja ambae hakuwa mwanafamilia  ambae alikuwa ni mpenzi wa mmoja w adada zake.

kundi la makoma lilipata umaarufu mkubwa sana sana kwasababu walijua kuimba lakini pia walitumia lugha tofauti tofauti kuimba ikiwemo kingereza, lingala na kifaransa tena kwa ufasaha kabisa.
alipokuw ana umri w amiaka 14 Nathalie alihamia  Netherlands pamoja na familia yake na kuanz akuchukua masomo ya maswala ya muziki jukwaani na namna ya ku imba  wkatika chuo cha Rockacademie huko  Tilburg.



wakati huohuo kundi la makoma lililuwa likiendelea kufanya matamasha kama kawaidana kuzunguka dnia nzima kwa matamasha wakati ambapo nathalie alikuwa ameacha kuambatana na kundi hilo na kujikita zaidi katika maswala yake ya elimu zaidi.


Mnamo mwaka 2002, kundi lao likashinda tunzo ya  Best African Music Group, kwenye  Kora South African Music Awards.na waliweza kupata mafanikio dunia nzima kutokana na kuimba muziki wa dini .
akiwa muimbaji kiongozi , Nathalie pia alijaribu sana kujiendeleza kimuziki na mwaka  2002  akaachia album yake ya kwanza waliyoiita On Faith (2002). album ambayo aliimba bado katika mahadhi ya dini.
Mwaka2004, akaikacha makoma moja kwa moja na kuhamakazi yake huko Englandshe na baadae akiwa nchini . mwaka  2005, akatoa album nyingine akiwa kama solo sna kuiita  I Saw the Light hii ilikuw ani album yake ya pili.

hivyo ndivyo alivyo anza mwana dada huyu mpaka hapo alipofika leo na kisha kuamua kuutosa muziki wa dini na kujikita zaidi katika muziki wa dunia .

                                                     Nathalie akiwa na mume wake.

Nathalie ameolewa  kama uonavyo pichani juu akiwa na mumewe na pia ni mama  nisikuchoshe ila kama unataka kufahamu zaidi juu ya mwana mama huyo basi niulize ntakujibu hapo nimekujuza kwa kifupi mmno mwana mama huyu ana mambo mengi mno kadri muda unavyozidi kwenda natakuwa nakujulisha zaidi.